6 Februari 2026 - 23:53
Reuters: Iran Yasisitiza Haki ya Kurutubisha Uranium Katika Mazungumzo ya Muscat

Reuters yaripoti kuwa Iran imesisitiza haki yake ya kurutubisha uranium katika mazungumzo ya Muscat, huku ikionyesha utayari wa kujadiliana kuhusu kiwango cha urutubishaji au kuanzishwa kwa consortium ya kikanda, na ikaongeza kuwa masuala ya makombora hayakujumuishwa kwenye ajenda ya mazungumzo.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Reuters: Iran Yasisitiza Haki ya Kurutubisha Uranium Katika Mazungumzo ya Muscat
Shirika la habari la Reuters, likinukuu chanzo cha kidiplomasia katika eneo hilo, limeripoti kuwa katika mazungumzo ya Muscat, Iran imesisitiza haki yake ya kurutubisha uranium, lakini ikaeleza iko tayari kujadiliana kuhusu kiwango cha urutubishaji au kuundwa kwa muungano (consortium) wa kikanda.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Tehran inaamini kuwa msimamo wake umeeleweka vyema nchini Marekani.
Reuters pia imeandika kuwa nchini Iran kuna mtazamo kwamba Marekani imeonyesha unyumbufu kuhusu baadhi ya madai ya Tehran, na kwamba uwezo wa makombora ya Iran haukujadiliwa katika mazungumzo hayo.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha